Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 26, 2024 Local time: 22:26

Novak Djokovic afukuzwa Australia


Novak Djokovic wa Serbia kati kati akijiandaa kuondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Melbourne Australia Januari 16, 2022, baada ya kushindwa katika vita kali ya kisheria kuhusu hali yake ya chanjo yake.
(Photo by Mell Chun / AFP)
Novak Djokovic wa Serbia kati kati akijiandaa kuondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Melbourne Australia Januari 16, 2022, baada ya kushindwa katika vita kali ya kisheria kuhusu hali yake ya chanjo yake. (Photo by Mell Chun / AFP)

Mchezaji maarufu wa Tennis Novak Djokovic aliondoka Australia leo Jumapili  baada ya kupoteza ombi lake la mwisho la kuzuia  kufukuzwa nchini humo na kushiriki katika michuano ya  Australian Open licha ya kutokuwa na chanjo ya COVID-19.

Awali mahakama kwa kauli moja ilitupilia mbali changamoto ya mchezaji huyo wa tenisi nambari 1 ya kufutwa kwa visa yake.

Djokovic, mwenye umri wa miaka 34 kutoka Serbia, alisema amesikitishwa sana na uamuzi huo lakini anauheshimu.

Mchezaji huyo akiwa amevaa barakoa alipigwa picha katika chumba cha mapumziko cha uwanja wa ndege wa Melbourne akiwa na maafisa wawili wa serikali waliovalia sare nyeusi. Aliondoka kwa ndege ya shirika la Emirates hadi Dubai, jiji lile lile la Umoja wa Falme za Kiarabu alikosafiri hadi Australia.

Djokovic ameshinda rekodi ya mataji tisa ya Australian Open, yakiwemo matatu mfululizo, lakini wakati huu hatapata nafasi ya kujaribu hilo.

XS
SM
MD
LG