Waziri wa mambo ya ndani wa Austria, Johanna Mikl-Leitner anasema njia ya wahamiaji ya Balkan itaendelea kufungwa baada ya Slovania, Macedonia, Serbia na Croatia kufunga mipaka wiki hii kwa wahamiaji wote wanaopanga kutafuta hifadhi ndani ya mipaka yao.
Mikl-Leitner ameliambia na gazeti la kila siku la Ujerumani la Die Welt leo kwamba njia ya Balkan kupitia nchi zote itaendelea kufungwa na kusema hawatarudi nyuma kwa uamuzi huo.
Wakati huohuo shirika la habari la Uturuki linasema wahamiaji watano, ikijumuisha mtoto mchanga wa miezi mitatu, wamezama katika ufukwe wa magharibi wa Uturuki baada ya boti iliyokuwa imewabeba kuelekea Uguriki kuzama ikiwa njiani kuelekea kisiwa cha Lesbos.