Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 18:01

Nigeria yapokea zaidi ya dozi milioni 4 za Covid kutoka Uhispania


Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari aonyesha hati ya kupokea chanjo ya Covid kwenye picha ya awali.
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari aonyesha hati ya kupokea chanjo ya Covid kwenye picha ya awali.

Nigeria imepokea dozi milioni 4.4 za Covid-19 chanjo aina ya Johnson & Johnson kutoka Uhispania, kulinaga na afisa mmoja wa ngazi ya juu serikalini.

Nigeria tayari imehaspokea dozi milioni 2 za chanjo ya Johnson & Johnson kutoka Finland, Ugiriki na Slovenia huku zaidi ikitarajiwa kutoka nchi za Umoja wa Ulaya.Faisal Shuaib, mkuu wa Wakala wa Kitaifa wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (NPHCDA), amesema kwamba lengo la Nigeria ka kuchanja asilimia 70 ya watu wake na kwamba sasa hilo litawezekana kutokana na mchango wa Uhispania.

Shuaib alisema 23.4 ya watu wanaostahili wamepata dozi ya kwanza ya chanjo, wakati asilimia 15.8 wakiwa wamechanjwa kikamilifu dhidi ya virusi vya corona. Nigeria imerekodi kesi 255,937 zilizothibitishwa kufikia Jumanne na vifo 3,143 tangu janga hilo kuzuka miaka miwili iliyopita.

XS
SM
MD
LG