Bodi mpya ya kusimamia mitihani nchini sasa imeteuliwa siku chache tu baada ya wanachama wa bodi ya kusimamia mitihani KNEC nchini Kenya kutimuliwa, na kuagizwa iandikishe taarifa za uchunguzi kwenye makao makuu ya polisi kuhusiana na wizi wa mitihani nchini humo.
Wakuu wa usalama wamekiri kuwa udanganyifu wa mitihani ya kitaifa umeongezeka kutokana na mitandao ya kijamii, baada ya matokeo ya wanafunzi 5,000 waliofanya mtihani mwisho wa mwak jana kufutiliwa mbali kama Josephat Kioko anavyoeleza kutoka Mombasa.