Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu ambaye amezungukwa na migogoro anakusudia kupata ushindi wa ajabu katika uchaguzi mpya Machi 2020 nchini Israeli.
Baada ya kushinda uchaguzi wa awali katika chama chake sasa anaweza kukiongoza chama chake cha mrengo wa kulia kuingia katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu.