Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Machi 22, 2025 Local time: 08:39

Ndege yazama Ziwa Nakuru Kenya


Ziwa Nakuru
Ziwa Nakuru

Kufuatia ajali ya ndege iliyoripotiwa asubuhi Jumamosi katika jimbo la Nakuru nchini Kenya, watu watano wanahofiwa kufariki baada ya ndege hiyo kuzama katika Ziwa Nakuru.

Seneta wa Nakuru Susan Kihika amethibitisha kuwa watu watatu walikuwa ni waandishi wa habari katika timu yake ya kampeni.

Ndege hiyo ya kibinafsi yenye usajili 5Y NMJ ilizama katika ziwa Nakuru muda mfupi baada ya kupaa karibu na hoteli moja kuwachakua abiria fulani wanaoripotiwa kuwa wanasiasa.

Kufuatia kuzama huko maafisa wa idara ya kudhibiti majanga nchini Kenya wanaeleza kuwa bado hawajafahamu sehemu ndani ya Ziwa hilo ambako mabaki ya ndege hiyo yapo.

Abiria watano, wanaume wanne na mwanamke mmoja wanaoripotiwa kuwa katika ndege hiyo hawafahamiki iwapo bado wangali hai.

Shughuli za uokoaji kutoka vitengo vyote vya usalama nchini Kenya vimefika katika eneo la mkasa.

XS
SM
MD
LG