Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 11:49

"NATO ya Waislam" yazinduliwa Saudi Arabia


Mrithi wa Ufalme Mohammed bin Salman
Mrithi wa Ufalme Mohammed bin Salman

Ushirika wa majeshi ya Waislam unaongozwa na Saudi Arabia, ambao kamanda wake ni mkuu wa majeshi ya Pakistan mstaafu umeanzishwa rasmi Jumapili huko mjini Riyadh ambapo mawaziri wa ulizindi wa nchi hizo wanakutana katika ufunguzi huo.

Wakati wanaounga mkono ushirika huo wameupa jina la “NATO ya Waislam,” lakini wadadisi pamoja na wale walioko Pakistan, wameendelea kuhoji malengo ya umoja huo na kuangalia kama ni kikundi kilichojikita katika madhehebu dhidi ya wapinzani wao -Mashia wa Iran, Syria na Iraq.

Mrithi wa Ufalme Mohammed bin Salman, ambaye pia ni waziri wa ulinzi wa Saudi Arabia, amefungua mkutano huo wa Umoja wa Majeshi ya Kiislam yanayopambana na ugaidi au kifupi chake IMCTC.

Tamko rasmi limeeleza kuwa “umoja huo wa nchi za Kiislam” ambazo ni 41 za madhehebu ya Kisuni zitaratibu na kugawana majukumu yao mmoja mmoja katika vita vya dunia dhidi ya ugaidi na uvunjifu wa amani uliopitiliza mipaka.

“Mkutano huo [unaofanyika mji mkuu wa Saudia unatimiza ahadi ya kuanzishwa rasmi kwa IMCTC na kuupa nguvu ushirikiano huo na muungano wa nchi wanachama katika ushirika huo,” taarifa hiyo imesema.

Maafisa wa Saudi Arabia walitangaza kuundwa kwa umoja huo mwaka 2015, wenye makao yake makuu Riyadh, ukiwa na lengo la kupambana na ugaidi, na hasa kukabiliana na tishio la kikundi cha Islamic State.

Lakini Tehran imepinga hatua hiyo kutokea mwanzoni kabisa, na imeendelea kuupinga katika duru mbalimbali, ikiamini kuwa lengo la ushirika huo wa Kisuni ni Saudi Arabia kupanua himaya yake katika eneo la Mashariki ya Kati.

Kuundwa kwa ushirika huo umekuwa ukiangazwa katika majadiliano yanayoendelea hasa Pakistan baada ya aliyekuwa mkuu wa majeshi wa Pakistani Raheel Sharif kuchaguliwa kuongoza taasisi hiyo ya IMCTC.

Wanaopinga hatua hiyo wamesema kuwa kushiriki kwa Islamabad katika ushirika huo unaweza kuwakasirisha jamii ya waliowachache wa madhehebu ya Kishia nchini humo na kuharibu mahusiano na Iran, ambayo inashirikiana katika mpaka wa kilomita 1,000 na Pakistan.

Baraza la Seneti la Pakistan lilishuhudia malumbano makali juu ya suala hili wiki iliyopita ambapo upinzani ulisisitiza kuwa serikali isishiriki katika shughuli za mkutano wa Jumapili Riyadh bila ya kupata idhini ya bunge.

XS
SM
MD
LG