Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Desemba 21, 2025 Local time: 12:15

Mwendesha mashtaka mkuu wa ICC aomba hati ya kukamatwa kwa Netanyahu na viongozi wa Hamas


Mwendesha mashtaka mkuu wa ICC Karim Khan
Mwendesha mashtaka mkuu wa ICC Karim Khan

Mwendesha mashtaka mkuu kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu Jumatatu amesema anataka kuomba hati ya kukamatwa kwa waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na waziri wa ulinzi Yoav Gallant, pamoja na kiongozi wa Hamas huko Gaza Yahya Sinwar kuhusiana na vita vya Israel na Hamas.

Karim Khan amesema katika taarifa kwamba ofisi yake inaamini Netanyahu na Gallant “wana jukumu la uhalifu wa kivita dhidi ya ubinadamu, ikiwemo kuwatesa raia na njaa kama mbinu ya kivita na kuagiza kwa makusudi mashambulizi dhidi ya raia.

“Ofisi yangu inahakikisha kwamba vitendo hivi vilifanyika kama sehemu ya mpango wa pamoja wa kutumia njaa kama mbinu ya kivita na vitendo vingine vya ukatili dhidi ya raia wa Gaza kama njia ya kuitokomeza Hamas, kuhakikisha kurudi kwa mateka waliotekwa na Hamas, na kuwaadhibu kwa pamoja wakazi wa Gaza, ambao wanadhaniwa ni tishio kwa Israel,” Khan amesema katika taarifa.

Mbali na Sinwar, Khan alisema kamanda wa tawi la kijeshi la Hamas Mohammed Diab Ibrahim al-Masri na mkuu wa ofisi ya kisiasa ya Hamas Ismail Haniyeh pia wanahusika na uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu.

Khan amesema tuhuma dhidi ya maafisa wa Hamas ni pamoja na mauaji, kuwashikilia mateka kama uhalifu wa kivita, ubakaji na ukatili mwingine wa kingono, na mateso.

Forum

XS
SM
MD
LG