Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 23, 2024 Local time: 19:30

Mwandishi wa vitabu wa Uganda aliyetoroka nchi yake, awasili Ujerumani kwa ajili ya matibabu


Mwandishi wa vitabu wa Uganda Kakwenza Rukirabashaija akifika mahakamani, katika shauri la kuomba arudishiwe pasipoti yake. Kampala, Februari 1, 2022, Picha ya AP.
Mwandishi wa vitabu wa Uganda Kakwenza Rukirabashaija akifika mahakamani, katika shauri la kuomba arudishiwe pasipoti yake. Kampala, Februari 1, 2022, Picha ya AP.

Mwandishi wa vitabu wa Uganda Kakwenza Rukirabashaija, aliyetoroka nchi baada ya kushtakiwa kwa kumutusi rais Yoweri Museveni na mwanawe amefarijika kuwasili Ujerumani ili kuweza kupata matatibabu baada ya kuteswa gerezani, wakili wake ameliambia shirika la habari la AFP leo Jumatano

Rukirabashaija amesema hakua katika hali ya usalama alipokua Afrika akihofia kwamba anaweza kurudishwa nyumbani kutokana na hali kwamba viongozi wa kimabavu barani humo hushirikiana pamoja.

Umoja wa Ulaya ni miongoni mwa washirika walioomba uchunguzi wa kina kuhusu vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Uganda.

Rukirabashaija aliyeachiliwa kwa dhamana amesema kwamba aliondoka Uganda kupitia Rwanda kwa mgu na kusafiri kupitia nchi ya tatu kabla ya kuwasili Ujerumani.

Wakili Eron Kiiza amesema bila kutoa maelezo zaidi kwamba baada ya hapo shirika la Umoja wa mataifa linalohudumia wakimbizi ( UNHCR) ndilo lilimusaidia kufika Ujerumani.

XS
SM
MD
LG