Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Februari 06, 2025 Local time: 15:10

Mwanafunzi auwa wanafunzi wenzake Florida


Wanafunzi wa shule ya Marjory Stoneman Douglas wakifuata maelekezo baada ya tukio
Wanafunzi wa shule ya Marjory Stoneman Douglas wakifuata maelekezo baada ya tukio

Mwanafunzi, aliyekuwa amefukuzwa shule ya sekondari ya Marjory Stoneman, Douglas huko Florida, nchini Marekani, kwa sababu ya ukosefu wa maadili alirudi kwenye majengo ya shule hiyo na akiwa na silaha Jumatano mchana na kuwauwa wanafunzi 17.

Mkuu wa polisi wa wilaya ya Broward, Scott Israel alieleza kwamba ilikuwa siku ya maafa mabaya kwa wilaya yake na kumtaja jina mtuhumiwa kwa shambulizi hilo la kikatili kuwa ni Nicolas Cruz.

Gavana wa jimbo la Florida Rick Scott akizungumzia tukio hilo
Gavana wa jimbo la Florida Rick Scott akizungumzia tukio hilo

Polisi walieleza mtuhumiwa alikamatwa nje ya uwanja wa shule bila ya kupambana. Mkuu wa polisi alisema Cruz alikua na risasi nyingi na bunduki mmoja. Israel anasema waaathirika 12 walifariki ndani ya shule, wengine watatu waliuliwa nje ya majengo ya shule na wawili walifariki kutokana na majeraha huko hospitali. Pia kuna watu wengine 14 waliojeruhiwa.

Rais wa Marekani, Donald Trump ameahidi kutoa msaada kwa wakuu wa Florida ili kusaidia katika maafa hayo yaliyotokea.

XS
SM
MD
LG