Mwanamke wa Kichina ambaye anafahamika kama malkia wa biashara haramu ya pembe za ndovu katika eneo la Afrika Mashariki leo amepanda kizimbani akikabiliwa na mashitaka ya kuendesha genge linaloratibu biashara hiyo.
Mtuhumiwa huyo Yang Feng Glan, akiwa sambamba na watuhumiwa wengine wawawili raia wa Tanzania walitiwa mbaroni hivi karibuni baada ya kuwindwa kwa muda mrefu katika vita ya kupambana na wafanya ujangili.
Mwandishi wetu Dar es salaam, George Njogopa amefuatilia mwenendo wa kesi hiyo inayoendelea jijini Dar es salaama alianda taarifa ambayo unaweza kuisikiliza hapo chini.