Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 15:28

Mshambuliaji wa Las Vegas atambuliwa


Hoteli ya Mandalay Bay Hotel, Las Vegas
Hoteli ya Mandalay Bay Hotel, Las Vegas

Watu 58 wamepoteza maisha na wengine zaidi ya 500 kujeruhiwa katika mji wa kitalii wa Las Vegas, Jimbo la Nevada, Marekani Jumapili katika shambulizi la kurusha risasi lililotokea wakati wa tamasha la muziki.

Mkuu wa polisi mjini Las Vegas, Joseph Lombardo, amewaambia waandishi wa habari kuwa mshambuliaji huyo alikuwa katika ghorofa ya 32 katika jengo la Mandalay Bay Casino, lilioko upande wa pili wa eneo la shambulizi.

Polisi wamemtambua mshambuliaji huyo kama Stephen Paddock, miaka 64, na wanaamini kwamba alifanya hivyo akiwa peke yake bila ya kushirikiana na mtu yoyote.

Mamlaka zimesema kuwa zinamhoji mwanamke mmoja ambaye anaaminiwa kuwa alikuwa anaishi na mshukiwa huyo.

Mshambuliaji huyo aliuuawa kwenye chumba chake cha hoteli na polisi wanasema wamegundua silaha kadhaa.

XS
SM
MD
LG