Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Mei 25, 2025 Local time: 05:33

Mpango wa kusafirisha nafaka ya Ukraine wapaswa kuendelea bila ushiriki wa Russia-Zelenskiy


Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy akifanya mkutano na waandishi wa habari wakati wa mkutano wa NATO mjini Vilnius, Lithuania, Julai 12, 2023
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy akifanya mkutano na waandishi wa habari wakati wa mkutano wa NATO mjini Vilnius, Lithuania, Julai 12, 2023

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy amesema makubaliano ya usafirishaji wa nafaka ya Ukraine kutoka Bandari ya Black Sea yanapaswa kuendelea kutekelezwa na kufanya kazi bila ushiriki wa Russia, baada ya Moscow kujitoa kwenye makubaliano hayo Jumatatu.

Zelenskiy alisema katika ujumbe wake wa kila usiku kwa njia ya video kwamba Ukraine ni chanzo cha chakula kwa watu milioni 400.

“Afrika ina haki kwa utulivu, Asia ina haki kwa utulivu,” alisema.

Russia Jumatatu ilisitisha ushiriki wake katika makubaliano hayo ya mwaka mmoja ambayo yanaruhusu Ukraine kuuza nje nafaka kupitia njia salama ya usafirishaji katika bahari ya Black Sea, na kusababisha wasiwasi katika nchi maskini kwamba bei zitapanda na kufanya iwe vigumu kuzimudu.

Moscow ilipendekeza kwamba ikiwa matakwa ya kuboresha mauzo ya nje ya nafaka na mbolea yake yatatekelezwa, itafikiria kufufua tena makubaliano hayo yanayojulikana kama mpango wa nafaka wa Black Sea.

Makubaliano hayo yaliyosimamiwa na Umoja wa Mataifa na Uturuki yalisifiwa kuwa yalizuia mzozo wa chakula duniani kufuatia uvamizi wa Russia dhidi ya Ukraine mwezi Februari 2022 na kufungwa kwa bandari za Black Sea.

“Ukraine, Umoja wa Mataifa na Uturuki kwa pamoja wanaweza kuhakikisha shughuli kwenye njia salama ya chakula na ukaguzi wa meli. Hii ni muhimu kwa ulimwengu mzima, Zelenskiy alisema.

Forum

XS
SM
MD
LG