Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 08:17

Mpaka kati ya Burundi na Rwanda umefunguliwa rasmi


Bango lenye maneno yaliyoandikwa katika lugha ya kirundi kuonyesha mpaka kati ya Rwanda na Burundi
Bango lenye maneno yaliyoandikwa katika lugha ya kirundi kuonyesha mpaka kati ya Rwanda na Burundi

Waziri wa mambo ya nje wa Burundi Albert Shingiro, amesema kwamba mpaka kati ya Burundi na Rwanda umefunguliwa rasmi.

Mpaka huo ulikuwa umefungwa kwa karibu miaka sita kutokana na sababu za kisiasa na baadaye kutokana na janga la virusi vya Corona.

Katika mkutano na waandishi wa habari mjini Burundi, waziri Albert Shingiro, amesema kwamba Burundi inaitaka Rwanda kuwarudisha watu waliokuwa wamepanga kutekeleza mapinduzi ya mwaka 2015.

Jaribio la mapinduzi la kutaka kumuondoa madarakani aliyekuwa rais wa nchi Pierre Nkurunziza. Jaribio hilo lilifeli.

Rwanda ilikuwa imetangaza kufungua mpaka wake na Burundi miezi kadhaa iliyopita.

XS
SM
MD
LG