Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 11:29

Moto mkubwa zaidi unaoteketeza misitu washindwa kudhibitiwa California


Gari la zimamoto likiwa katika njia kuu namba 96 huku moto ukiendelea kuteketeza Msitu wa Taifa wa Klamath huko California, July 30, 2022.
Gari la zimamoto likiwa katika njia kuu namba 96 huku moto ukiendelea kuteketeza Msitu wa Taifa wa Klamath huko California, July 30, 2022.

Msemaji wa idara ya kitaifa ya misitu, Aderienne Freeman, amesema kwamba moto mkubwa unaendela kuteketeza sehemu za Mckinney, katika msitu wa kitaifa wa Klamath, North Carolina.

Ukubwa wa moto huo umeongezeka na kuenea hadi umbali wa kilomita 207 mraba, siku mbili baada ya kuripotiwa katika kaunti ya Siskiyou, yenye idadi ndogo ya watu.

Uchunguzi unaendelea kubaini kilichosababisha moto huo.

XS
SM
MD
LG