Msemaji wa polisi katika maeneo ya Kampala Luke Owesingire, amesema kwamba moto huo umetokea saa saba usiku wakati wanafunzi walikuwa wamelala.
“Kufikia sasa, watu 11 wamefariki dunia kutokana na moto huo. Watu 6 wapo katika hali mahtuti wakitibiwa katika hospitali ya Herona,” amesema Owesingire.
Polisi wanachunguza kilichosababisha moto huo.