Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Februari 10, 2025 Local time: 04:22

Morales azuiwa kugombea urais Bolivia


Aliyekuwa rais wa Bolivia Evo Morales
Aliyekuwa rais wa Bolivia Evo Morales

Mahakama ya kikatiba nchini Bolivia imemzuia rais wa zamani Evo Morales kugombea urais kwa mara nyingine, hatua ambayo imeitumbukiza zaidi nchi hiyo katika mgogoro wa kisiasa ambao umekuwa ukiendelea kwa muda mrefu.

Morales, ambaye aliiongoza Bolivia kati ya m waka 2006 na 2019, amekuwa akigombea uongozi wa chama chake cha MAS, akikabiliwa na ushindani kutoka kwa aliyekuwa mwandani wake ambaye ni mpinzani mkubwa, rais Luis Arce.

Lakini hatua ya wiki iliyopita, ambayo iliripotiwa Ijumaa, ya mahakama ya kikatiba kuamua kwamba marais wanastahili kuhudumu kwa mihula miwili pekee iwe ni mihula inayofuatana au la.

Baada ya kuhudumu kwa mihula miwili ya kwanza, uamuzi wa mahakama ulimruhusu Morales kuhudumu kwa muhula wa tatu baada ya mabadiliko ya katiba.

Aligombea muhula wa nne mwaka 2019 lakini akatoroka nchini kufuatia ghasia za baada ya uchaguzi.

Forum

XS
SM
MD
LG