Polisi mjini Mombasa huko Kenya wanachunguza mienendo ya vijana wadogo wanaodaiwa kujihusisha na uhalifu na kuhangaisha raia katika mji huo kwa kuwashambulia kwa silaha hatari na hata kuwaibia.
Vyombo vya usalama eneo hilo la Pwani vinawazuia vijana 17 waliokamatwa mwishoni mwa wiki, miezi michache baada ya magenge yanayotumia majina tofauti kuchipuka na mbinu kama hiyo.
Mwandishi wetu Josephat Kioko ameandaa taarifa zaidi..