Lakini haikuwekwa wazi kama makundi ya kibinadamu yataweza kupata misaada kwa sababu ya mapigano yanayoendelea katika eneo hilo.
Misri inakataa kufungua tena upande wake wa mpaka wa Rafah hadi udhibiti wa upande wa Gaza utakaporejeshwa kwa Wapalestina.
Ilikubali kuelekeza misafara kwa muda kupitia mpaka wa Kerem Shalom wa Israel, ambacho ni kituo kikuu cha mizigo kwa Gaza, baada ya mazungumzo kati ya Rais wa Marekani, Joe Biden na Rais wa Misri Abdel-Fattah el-Sissi.
Lakini kivuko hicho kwa kiasi kikubwa hakipitiki kwa sababu ya mapigano yanayohusishwa na mashambulizi ya Israel katika mji wa karibu wa Rafah.
Forum