"Natumai kwamba EU inaweza kweli kuchukua hatua madhubuti ili kumrudisha Ahmadreza nyumbani," Vida Mehrannia alisema kulingana na sehemu ya mahojiano kwenye idhaa ya ZDF ya Ujerumani.
EU lazima "isiruhusu mtu asiye na hatia kuuawa kwa njia hiyo ya kinyama", aliongeza.
Djalali alihukumiwa kifo mwaka 2017 kwa tuhuma za ujasusi, tuhuma zilizokanushwa na Sweden na wafuasi wake.