Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 30, 2025 Local time: 10:23

Miji kadhaa ya China yaondoa masharti makali ya kukabiliana na Covid


Polisi wa kukabiliana na ghasia katika mavazi ya kujikinga na maambukizi ya Covid wanaonekana mtaani wakati wa maandamano ya kupinga masharti makali ya kukabiliana na Covid, mjini Guangzhou, Novemba 29, 2022
Polisi wa kukabiliana na ghasia katika mavazi ya kujikinga na maambukizi ya Covid wanaonekana mtaani wakati wa maandamano ya kupinga masharti makali ya kukabiliana na Covid, mjini Guangzhou, Novemba 29, 2022

Miji kadhaa kote China leo Ijumaa imeanza kuondoa masharti makali ya kukabiliana na maambukizi ya Covid 19, na hivyo kulegeza masharti ya upimaji na karantini kufuatia maandamano makubwa ya kitaifa ya kutaka masharti hayo yafutwe kabisa na na kuwepo uhuru wa kisiasa.

Hasira iliongezeka kutokana na hatua kali za China katika kukabiliana na janga la covid na kupelekea watu kumiminika mitaani mwishoni mwa Jumaa lililopita katika maandamano makubwa ambayo hayajawahi kushuhudiwa kwa miongo kadhaa.

Kufuatia machafuko yaliyotokea kote China, mijii kadhaa imeanza kulegeza masharti ya kupambana na Covid, kama vile kuondoa masharti ya kulazimisha upimaji wa watu wengi kila siku, ambao ulikuwa msingi wa maisha ya kila siku chini ya sera kali ya Beijing ya kutopatikana hata kisa kimoja cha maambukizi ya Covid.

Kuanzia leo, mji mkubwa wa kusini magharibi wa Chengdu hautalazimisha tena watu kuonyesha kwamba walipimwa na hawakukutwa na maambukizi ili waruhusiwe kuingia kwenye maeneo ya umma au kusafiri na treni ya mwendo kasi, maarufu metro.

XS
SM
MD
LG