Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 02:11

Mfumuko wa bei waongezeka Afrika Kusini


Maandamano ya Mfumuko wa Bei Afrika Kusini.
Maandamano ya Mfumuko wa Bei Afrika Kusini.

Mfumuko wa bei nchini Afrika Kusini uliongezeka hadi kiwango cha juu zaidi katika kipindi cha miaka 13 mwezi Julai, ukisukumwa zaidi na kupanda kwa bei za vyakula, usafiri na umeme, data rasmi ilionyesha Jumatano wakati wafanyakazi wakifanya maandamano kupinga gharama kubwa ya maisha.

Bei za bidhaa zilipanda kwa kiwango cha kila mwaka cha asilimia 7.8 mwezi Julai, kutoka asilimia 7.4 mwezi Juni, shirika la takwimu la taifa la StatsSA lilisema katika taarifa yake.

Kuchapishwa kwa takwimu za hivi karibuni kuliendana na maandamano katika miji mikubwa kuhusu hali mbaya ya uchumi, ambayo imekuwa ikikandamiza watu maskini zaidi katika nchi iliyoendelea zaidi kiviwanda barani.

Waandamanaji wakiongozwa na vyama viwili vikubwa zaidi vya wafanyakazi nchini Afrika Kusini walitoa wito kwa serikali kuchukua hatua kukabiliana na ongezeko la umaskini na gharama ya maisha katika nchi hiyo isiyo na usawa zaidi duniani.

XS
SM
MD
LG