Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Januari 16, 2025 Local time: 19:22

Mfalme Frederik X apewa kiti cha ufalme Denmark


Mfalme wa Denmark Frederik X na Malkia Mary wa Denmark wakipita katikati ya umati kwenye gari lao walipokuwa wakiondoka kwenye Kasri la Christiansborg huko Copenhagen, Denmark, Jumapili, Januari 14, 2024.
Mfalme wa Denmark Frederik X na Malkia Mary wa Denmark wakipita katikati ya umati kwenye gari lao walipokuwa wakiondoka kwenye Kasri la Christiansborg huko Copenhagen, Denmark, Jumapili, Januari 14, 2024.

Mfalme wa Denmark Frederik X alipewa kiti cha ufalme siku ya Jumapili, akimrithi mama yake, Malkia Margrethe II, ambaye alijiuzulu rasmi baada ya miaka 52 ya Umalkia, huku umati mkubwa wa watu ukikusanyika katika mji mkuu kushuhudia historia.

Margrethe mwenye umri wa miaka 83, alilishangaza taifa katika mkesha wa mwaka mpya alipotangaza kuwa amepanga kuwa kiongozi wa kwanza wa ufalme wa Denmark katika takriban miaka 900 kuachia kiti cha enzi kwa hiari.

Mfululizo huo ulirasimishwa wakati Margrethe alipotia saini tamko la kuachia umalkia wakati wa mkutano wa Baraza la Taifa katika bunge, ikulu ya kifalme ilisema. Denmark, mojawapo ya mataifa ya kale zaidi ya kifalme duniani, hawana hafla ya kutawazwa.

Forum

XS
SM
MD
LG