Margrethe mwenye umri wa miaka 83, alilishangaza taifa katika mkesha wa mwaka mpya alipotangaza kuwa amepanga kuwa kiongozi wa kwanza wa ufalme wa Denmark katika takriban miaka 900 kuachia kiti cha enzi kwa hiari.
Mfululizo huo ulirasimishwa wakati Margrethe alipotia saini tamko la kuachia umalkia wakati wa mkutano wa Baraza la Taifa katika bunge, ikulu ya kifalme ilisema. Denmark, mojawapo ya mataifa ya kale zaidi ya kifalme duniani, hawana hafla ya kutawazwa.
Forum