Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 17, 2025 Local time: 17:22

Meli ya kivita ya Marekani yatia nanga Korea Kusini kujibu Korea Kaskazini


Meli ya kubeba ndege ya Marekani, imewasili Korea Kusini, Jumapili katika kuonyesha uwepo wa nguvu ya kijeshi, siku chache baada ya Korea Kaskazini kufanya majaribio ya makombora ili kuonyesha uwezo wake wa kukabiliana na mashambulizi.

Kuwasili kwa USS Carl Vinson na kundi lake la mashambulizi katika bandari ya Korea Kusini ya Busan kulikusudiwa kuonyesha muungano thabiti wa kijeshi wa Marekani na Korea Kusini licha ya vitisho vinavyoendelea vya Korea Kaskazini, na kuongeza ushirikiano wa mali zote za washirika, jeshi la wanamaji la Korea Kusini limesema katika taarifa.

Kutumwa kwa meli hiyo kunatarajiwa kuikasirisha Korea Kaskazini, ambayo inaona nguvu hizo za kijeshi za Marekani kama vitisho kwa usalama.

Korea Kaskazini imejibu baadhi ya matukio ya siku za nyuma ya meli za kubeba ndege za Marekani, mabomu ya masafa marefu na nyambizi zinazotumia nyuklia kwa majaribio ya makombora.

Forum

XS
SM
MD
LG