Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Februari 13, 2025 Local time: 09:34

McMaster aonya uwezekano wa vita na Korea Kaskazini 'unaongezeka'


Mshauri wa usalama wa Taifa wa Marekani H.R. McMaster akizungumza na waandishi habari
Mshauri wa usalama wa Taifa wa Marekani H.R. McMaster akizungumza na waandishi habari

Mshauri wa usalama wa taifa wa White House amesema kuwa uwezekano wa kutokea vita na Korea Kaskazini yenye silaha za kinyuklia “unaongezeka kila siku”

“Kuna njia mbalimbali za kukabiliana na tatizo hilo ukiachilia mbali mapambano ya kijeshi,” H.R McMaster amesema Jumamosi.

“Lakini ni kukimbizana kwa sababu anakaribia karibu zaidi na zaidi na hakuna muda uliosalia,” akimkusudia katika maelezo yake kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un," amesema.

Korea Kaskazini imetangaza wiki iliyopita kuwa hivi sasa inaweza kuipiga nchi ya Marekani kwa kombora, baada ya kufanya jaribio la kombora jipya la balistika lenye uwezo wa kufika katika mabara mengine.

Taarifa za vyombo vya habari zinasema kuwa Pentagon inatizama maeneo ya magharibi mwa pwani ya Marekani ambako mifumo ya kujihami inaweza kuwekwa, kufuatia tishio la Korea Kaskazini kwamba itaipiga Marekani

Shirika la habari la Reuters limesema kuwa ulinzi huo wa kujihami utahusisha kuwekwa mitambo ya kuzuia makombora ya balistika yenye urefu kwenda juu kama ile iliyokuwa imewekwa Korea Kusini.

XS
SM
MD
LG