Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 02:15

Mchezaji wa Brazil akamatwa kwa tuhuma za unyanyasaji wa ngono


Mchezaji wa Brazil Dani Alves akisikiliza swali wakati wa mkutano na waandishi wa habari kabla ya mechi ya Kundi G ya Kombe la Dunia la Qatar kati ya Brazil na Cameroon, mjini Doha, Qatar, Desemba 1, 2022. AP
Mchezaji wa Brazil Dani Alves akisikiliza swali wakati wa mkutano na waandishi wa habari kabla ya mechi ya Kundi G ya Kombe la Dunia la Qatar kati ya Brazil na Cameroon, mjini Doha, Qatar, Desemba 1, 2022. AP

Sintofahamu imetanda kwa wapenzi wa soka ulimwenguni baada ya mchezaji soka wa Brazil Dani Alves kukamatwa siku ya Ijumaa baada ya kushutumiwa kwa kumnyanyasa  kingono mwanamke mmoja nchini Uhispania.

Kitendo hicho kinadaiwa kufanyika tarehe 31 Desemba katika klabu ya usiku mjini Barcelona, polisi wliliambia shirika la habari la Associated Press.

Alves sasa atafikishwa mbele ya jaji ambaye ataamua juu ya mashtaka hayo.

Shtaka la unyanyasaji wa kijinsia nchini Uhispania linaweza kumaanisha chochote kuanzia kupapasa kingono bila ridhaa ya mtu, kumshika kwa nguvu hadi ubakaji.

Polisi walisema hawakuweza kutoa maelezo zaidi kuhusu kesi hiyo.

Alves mwenye umri wa miaka 39 ni mmoja wa wachezaji waliofanikiwa zaidi katika kandanda, akishinda mataji makubwa na vilabu kadhaa vya juu vikiwemo Barcelona, Juventus na Paris Saint-Germain. Kwa sasa anachezea klabu ya Pumas ya Mexico.

XS
SM
MD
LG