Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 15, 2025 Local time: 05:48

Mchekeshaji wa Sudan Kusini awasihi wapiganaji kuwacha silaha


Wapiganaji wa Sudan Kusini kwenye picha ya maktaba
Wapiganaji wa Sudan Kusini kwenye picha ya maktaba

Mchekeshaji aliyewahi kuwa mwanajeshi mtoto huko Sudan kusini, amesema azma yake sasa ni kuwapa tabasamu watu waliotiwa kiwewe kwa miaka mingi kutokana na mapigano wakati pia na kutoa mafunzo kwa wanajeshi kuhusu namna ya kutangamana na raiya.

Kuech Deng Atem mwenye umri wa miaka 26 anasema kuwa matumaini yake ni kuwarai wapiganaji kuweka silaha chini kupitia vichekesho vyake, kwa kuwa mara nyingi wanatumia uwezo wao kupora mali na fedha kutoka kwa raiya.

Atem ambaye jina lake la kisanii ni Wokii Jeesh Commando, aliandikishwa kuwa mpiganaji akiwa na umri wa miaka 10.Yeye na watoto wenzake walipata mafunzo kwenye kambi za Aweil na Mapel na kisha baadaye kujiunga kwenye mapigano huko Heglig na Abyei mwaka 2012.

Anasema kwamba mwanzoni walitwikwa jukumu la kuwauguza wanajeshi waliojeruhiwa pamoja na kubeba silaha. Mwaka 2008, mama yake alimfuata huko Mapel na kisha kurudi naye Juba ambako alianza tena masomo.

XS
SM
MD
LG