Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 18:36

Mazungumzo ya kusitisha vita Ukraine yanaendelea


Waokoaji wa Ukraine wakiwa wamebeba mama mzee kumtpa chini ya daraja lililoharibiwa kutokana na mashambulizi ya Russia. April 1 2022
Picha: AP
Waokoaji wa Ukraine wakiwa wamebeba mama mzee kumtpa chini ya daraja lililoharibiwa kutokana na mashambulizi ya Russia. April 1 2022 Picha: AP

Ukraine imesema kwamba mazungumzo ya amani kati yake na Russia yameendelea kupitia njia ya video, baada ya wajumbe wake kukutana kwa mazungumzo ya moja kwa moja jumanne wiki iliyopita, mjini Istanbul.

Uturuki imeimarisha juhudi zake za kidiplomasia baada ya kile kimetajwa kama kupatikana mafanikio fulani katika mazungumzo ya jumanne.

Bila kutoa maelezo zaidi, ofisi ya rais wa Ukraine imesema kwamba maafisa wa Russia na Ukraine wamefanya mazungumzo kwa njia ya video.

Katika mahojiano ya televisheni, waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Mevlut Cavusoglu, amesema kwamba juhudi zinaendelea kuchukuliwa kutatua vita vya Ukraine, akisema kwamba Russia imekubali baadhi ya mapendekezo ya kusitisha vita japo haijatekeleza ahadi hiyo.

Amesema kwamba anaendeela kuwasiliana na mawaziri wa nchi za nje wa nchi hizo mbili kuhakikisha kwamba vita hivyo vinasitishwa.

XS
SM
MD
LG