Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 23, 2023 Local time: 02:35

Mazoezi yalioandaliwa na jeshi la Marekani Ghana yalenga kuimarisha ujuzi wa vikosi vya Afrika Magharibi


Wanajeshi wa Cabo Verde wakipa mafunzo wakati wa mpango wa kila mwaka wa kukabiliana na ugaidi unaoitwa "Operesheni Flintlock", huko Sogakope, Ghana Machi 14, 2023. REUTERS

Wanajeshi wa Afrika Magharibi walizivuta kwa utaratibu boti zao hadi kwenye eneo la kivuko kilichokuwa na kutu na kuziweka upande  ili kuwapokonya silaha waliokuwa kama watekaji nyara katika  moja ya mazoezi yao ya kijeshi.

Mazoezi hayo katika mto Volta nchini Ghana siku ya Jumamosi yalifanywa wakati wa mazoezi ya kwanza kabisa ya baharini yaliyoandaliwa na jeshi la Marekani chini ya mpango wake wa muda mrefu wa Flintlock ili kuimarisha ujuzi wa vikosi vya Afrika Magharibi.

Mafunzo hayo ya baharini katika nusu ya kwanza ya Machi yalikamilika kwa wanajeshi kukamata bunduki zao juu walipokuwa wakivuka kwenye mawimbi makubwa ya maji kabla ya kuvamia eneo la mapumziko la ufuo ili kutatua mgogoro wa mateka. Wakuu wa kijeshi na wanadiplomasia walitazama kwa karibu.

Admirali Milton Sands, kamanda wa Kamandi Maalum ya Operesheni ya Marekani kwa Afrika (SOCAF), alisema mpango huo umepanuka ili kuyasaidia mataifa ya pwani katika eneo hilo kukabiliana na vitisho vya baharini kama vile uharamia na uvuvi haramu.

Uvuvi haramu ni jambo muhimu ambalo tunajaribu kulifanyia kazi na washirika wetu ili kulipunguza kasi aliiambia Reuters siku ya Jumanne.

Facebook Forum

XS
SM
MD
LG