Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 06:16

Zoezi la Marekani, Seoul laibua wasiwasi


Mazoezi ya kivita
Mazoezi ya kivita

Wakati Marekani na Korea Kusini wanaanza zoezi kubwa zaidi la pamoja la kijeshi Jumatatu, maswali yameibuka iwapo jaribio la hivi karibuni la kombora lililofanywa na Korea Kaskazini limevuka "mstari mwekundu".

Kuvuka huko mstari huo ni uwezo wa Korea Kaskazini wa kusafirisha bomu lenye kichwa cha nyuklia na hatua gani zichukuliwe kudhibiti hali hiyo.

Mazoezi hayo ya kila mwaka ambayo hudumu kwa siku tano yenye jina ACE yanahusisha zaidi ya ndege za kijeshi 230 pamoja na wanajeshi 12,000 wa Marekani wanaoungana na wanajeshi wa Korea Kusini.

Ingawa mazoezi kama hayo huwa yamepangwa siku nyingi, zoezi la safari hii limeanza chini ya kipindi cha wiki moja baada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio la silaha ya masafa marefu yenye uwezo wa kubeba kichwa cha nyuklia, jambo ambalo marekani imesema halikubaliki.

Jesha la anaga la korea kusini limesema zoezi hilo litahusisha mashambulio yanayofanana na kushambulia vituo vya nuklia vya Korea Kaskazini na makombora yake. .

XS
SM
MD
LG