Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Oktoba 04, 2023 Local time: 12:51

Mazishi ya mabaki ya Lumumba yafanyika Kinshasa


Msafara uliobeba mabaki ya Patrice Lumumba ukiwasili mjiji Kinshasa mapema Juni 27, 2022

Mabaki ya aliyekuwa waziri mkuu wa kwanza wa Congo Patrice Lumumba yamezikwa lAlhamisi mjini Kinshasa kwenye eneo maalum lililojengwa , wakati rais Felix Tshisikedi akitoa hotuba yake.

Kwa mujibu wa shirika la habari la AP, hafla hiyo imefanyika wakati wa maadhimisho ya siku ya uhuru ambapo siku kama hii mwaka wa 1960 . taifa hilo lilijipatia uhuru wake kutoka Ubelgiji.

Lumumba anakumbukwa kama shujaa wa kitaifa aliyesaidia kumaliza utawala wa kikoloni. Lumumba alifanyika waziri mkuu wa Congo baada ya uhuru lakini akauwawa kabla ya kumaliza mwaka mmoja madarakani mwaka wa 1961.

Mazishi ya Alhamisi yamefanyika baada ya Ubelgiji kurejesha mabaki yake nchini mapema mwezi huu. Jeneza lililokuwa na jino lake awali lilipelekwa kwenye sehemu tofauti za nchi , ili kutoa nafasi kwa wananchi kutoa heshima zao kikiwemo kijiji alikozaliwa cha Onalua,kilichoko kwenye jimbo la Sankuru.

XS
SM
MD
LG