Mkataba huo unahusisha upunguzaji wa hiari kati ya Agosti na Machi, na utaruhusu nchi wanachama kukusanya vifaa kabla ya miezi ijayo ya msimu wa baridi.
Ikiwa kutakuwa na dharura, EU inaweza kufanya kupunguzwa huko kwa lazima, ingawa kwa misamaha fulani ambayo ilikubaliwa kama sehemu ya maelewano ili kufikia makubaliano.
Makubaliano hayo pia yanakuja huku kukiwa na matarajio kwamba Russia itakata usambazaji wa gesi kwa Umoja wa Ulaya kujibu vikwazo vya Umoja huo dhidi ya Russia kwa uvamizi wake wa Ukraine.