Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Januari 16, 2025 Local time: 07:46

Mataifa tajiri yalipa ahadi yao ya dola vilioni 100 kwa ajili ya mazingira


Mataifa tajiri yamekamilisha mpango wa malipo ya dola za kimarekani bilioni 100 ya ahadi ya fedha za kushughulikia hali ya hewa kwa nchi zinazoendelea na kuundaa mfuko wa kulinda mazingira ya viumbe na mimea na ulinzi wa misitu, Rais wa Ufaransa amesema Ijumaa. 

Rais Emmanuel Macron, amezungumza kwenye jopo la mwisho katika kilele cha mkutano mjini Paris ambapo baadhi ya viongozi 40, ikiwa ni pamoja na dazeni mbili kutoka Afrika, waziri mkuu wa China na rais wa Brazil walikutana ili kutoa msukumo kwa ajenda mpya ya fedha duniani.

Lengo la mkutano huo ni kuongeza ufadhili wa migogoro katika mataifa ya kipato cha chini na kupunguza mzigo wa madeni yao, kurejesha hali ya kawaida mifumo ya kifedha baada ya vita na kutoa fedha za kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa kwa kupata maelewano ya hali ya juu ya jinsi ya kukuza idadi ya mipango katika mashirika kama G20, COP, shirika la fedha la kimataifa – IMF, Benki ya Dunia, na Umoja wa Mataifa.

Forum

XS
SM
MD
LG