Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Januari 24, 2025 Local time: 01:38

Mashirika ya haki za binadamu yaitaka Iran kusitisha adhabu ya kifo


Mashirika ya kimataifa ya kutetea haki za binadamu yametoa wito wa shinikizo la kimataifa kwa Iran kuacha kutoa hukumu ya kifo kwa waandamanaji wanaoipinga serikali.

Mahakama ya Iran imesema watu watano waliokamatwa katika harakati ya serikali ya kukabiliana na maandamano ya miezi miwili wamehukumiwa kifo tangu Jumapili.

Wafungwa hao watano, ambao hakuna hata mmoja wao aliyetajwa, ni pamoja na watu watatu ambao walihukumiwa kifungo hicho Jumatano.

Katika ujumbe uliotumwa kwa VOA, Mahmood Amiry-Moghaddam, mkurugenzi wa shirika la Haki za Binadamu la Oslo la Iran, alisema serikali ya Iran inatumia hukumu ya kifo kujaribu kuwatia hofu wananchi kwa mara nyingine tena kuogopa mamlaka yake.

XS
SM
MD
LG