Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 21, 2025 Local time: 01:31

Mashambulizi ya Russia kwenye mji wa Ukraine wa Odesa yaua watu watatu


Jengo la makazi ya raia lililoharibiwa na makombora ya Russia, katika mji wa Odesa, Julai 1, 2022
Jengo la makazi ya raia lililoharibiwa na makombora ya Russia, katika mji wa Odesa, Julai 1, 2022

Russia ilifyatua makombora na kurusha ndege zisizo na rubani kwenye maeneo tofauti kote nchini Ukraine mapema Jumamosi, na kuua raia watatu katika mji wa bandari ya Black Sea wa Odesa na kushambulia uwanja wa ndege wa kijeshi katika mkoa wa kati wa Poltava, maafisa wa Kyiv wamesema.

Mashambulizi hayo, ambayo mtu mwenye umri wa miaka 29 aliuawa pia katika mkoa wa kaskazini mashariki wa Kharkiv kulingana na maafisa, ni ya hivi karibuni katika mfululizo wa mashambulizi ya usiku yaliyofanywa na Russia, wakati Kyiv ikiweka nguvu zake kwenye mashambulizi ya kujibu.

Jeshi la anga la Ukraine limesema makombora manane ya kutoka ardhini na ndege zisizo na rubani 35 zilitumiwa katika mashambulizi hayo. Vituo vya ulinzi wa anga vilifanikiwa kuangusha ndege 20 zisizo na rubani na makombora mawili ya baharini, jeshi hilo limesema.

“Kutokana na mapigano hayo ya angani, mabaki kutoka kwa moja ya ndege zisizo na rubani yalianguka kwenye ghorofa ya juu ya jengo la makazi ya raia na kusababisha moto,” msemaji wa jeshi eneo la kusini Natalia Humeniuk amesema kuhusu shambulio hilo kwenye mji wa Odesa.

Maafisa wa Ukraine wamesema watu watatu waliuawa wakiwemo wanandoa waliokuwa wanaishi kwenye ghorofa ya nane ya jengo hilo na mwanaume aliyekuwa nje wakati wa shambulio hilo.

Forum

XS
SM
MD
LG