Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Januari 13, 2025 Local time: 12:46

Mashambulizi ya anga ya Israel yaua watu 12 Ukanda wa Gaza


Jengo lililoharibiwa na shambulizi la Israel huko Deir el-Balah, katikati mwa Ukanda wa Gaza, Disemba 14, 2024. Picha ya AFP
Jengo lililoharibiwa na shambulizi la Israel huko Deir el-Balah, katikati mwa Ukanda wa Gaza, Disemba 14, 2024. Picha ya AFP

Madaktari Jumatano wamesema mashambulizi ya anga ya Israel yameua watu 12 katika Ukanda wa Gaza. Mashambulizi hayo ni pamoja na shambulizi lililofanyika katika mji wa Beit Lahiya, kaskazini mwa Gaza, ambalo liliua watu 10, madaktari wamesema.

Mashambulizi hayo ni pamoja na shambulizi lililofanyika katika mji wa Beit Lahiya, kaskazini mwa Gaza, ambalo liliua watu 10, madaktari wamesema.

Mashambulizi mengine ya Israel yalilenga eneo la Katikati mwa Gaza na Rafah kusini mwa Palestina.

Ghasia hizo zimetokea wakati kukiwa na juhudi mpya za kufikia makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na kundi la wanamgambo la Hamas ambayo yatajumuisha kuachiliwa kwa mateka ambao bado wanashikiliwa na wanamgambo hao huko Gaza.

Maafisa wa Israel walisema katika siku za hivi karibuni wana matumaini ya kufikia hatua katika mazungumzo ya muda mrefu yaliyokwama, huku Hamas ikisema Jumanne inaamini makubaliano yanawezekana ikiwa Israel haitaleta masharti mapya.

Forum

XS
SM
MD
LG