Mashambulizi ya Israel katika sehemu ya kusini mwa Rafah yamepelekea maelfu ya watu kuondoka sehemu hiyo ambayo imekuwa ikikaliwa na watu milioni 2.3 waliokimbia vita.
Njia kuu zilizokuwa zikitumika kusafirisha misaada kuingia Gaza zimefungwa, hatua ambayo imepelekea wasiwasi wa kutokea vifo vya watu kadhaa na njaa.
Israel imesema kwamba haina jingine la kufanya kando na kuushambulia mji huo ili kuwamaliza wanamgambo wa Hamas wanaoaminika kujificha Rafah.
Wakaazi wa Rafah wamesema kwamba ndege zisizokuwa na rubani za Israel zimeshambulia kitongozi cha Yibna usiku wa kuamkia leo na kupiga boti za uvuvi, baadhi zimewaka moto kwenye ufuo wa Rafah. Jeshi la Isral halijatoa taarifa kuhusu operesheni yake ndani ya Rafah.
Forum