Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 21, 2025 Local time: 02:37

Marufuku ya kutotoka nje inaendelea lutekelezwa Shanghai


Mji mtupu wakati wa utekelezaji wa marufuku ya kutotoka nje mjini Shanghai. May 16 2022. Picha: Reuters
Mji mtupu wakati wa utekelezaji wa marufuku ya kutotoka nje mjini Shanghai. May 16 2022. Picha: Reuters

Sehemu kubwa ya mji wa Shanghai imeendelea kufungwa kwa shughuli za kawaida, huku maafisa wakiendelea kupima watu ili kudhibithi maambukizi ya virusi vya Corona.

Wilaya ya Jing'an, katikati mwa Shanghai imeingia siku ya tatu ya shughuli zote kusitishwa kabisa isipokuwa usafirishaji wa bidhaa muhimu.

Shughuli ya upimaji ilifanyika mara tatu wakati shughuli za kawaida zimesitishwa, na watu kuruhusiwa kuondoka nyumbani wanapoenda kupimwa.

Maafisa wanaendelea kutoa chanjo dhidi ya Covid mjini humo wakilenga zaidi watu wazee.

XS
SM
MD
LG