Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 03:43

Marekani yasitisha huduma ya kutoa visa kwa Uturuki


Wizara ya mambo ya nje ya Marekani.
Wizara ya mambo ya nje ya Marekani.

Ubalozi wa Marekani huko Ankara nchini Uturuki umeeleza kwamba Marekani imesitisha kwa muda maombi yote ya visa za wasiotaka uhamiaji kutoka uturuki.

Taarifa ya ubalozi Jumapili inaeleza kwamba kufuatia matukio ya karibuni yalilazimisha serikali ya Marekani kutathmini tena dhamira ya dhati ya serikali ya Uturuki kwa usalama wa ofisi zake za ubalozi na wafanyakazi. Taarifa haikuelezea sababu zinazopelekea kutathmini tena dhamira ya uturuki wala haikusema usitishaji huo wa utoaji visa utadumu kwa muda gani.

Mfano wa Visa ya Marekani
Mfano wa Visa ya Marekani

Hata hivyo taarifa iliongeza ili kupunguza idadi ya wageni kwenda ubalozi wetu na ubalozi mdogo wakati tathmini inaendelea kuanzia sasa wamesitisha kwa muda huduma zote za visa za wasio taka kibali cha uhamiaji kwenye ubalozi wetu mdogo huko Uturuki.

Saa kadhaa baadae Uturuki nayo ilijibu kwa kutangaza usitishaji wake wa huduma za visa kwa wa-Marekani.

XS
SM
MD
LG