Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Januari 16, 2025 Local time: 08:04

Marekani yasema haihusiki na mauaji ya madaktari wa Cuba, Somalia


Jeshi la Marekani linasema halijahusika na mauaji ya madaktari wawili wa Cuba, ambao kundi la wanamgambo wa al-Shabab, linadai walikufa kwa shambulizi la anga la Marekani, nchini Somalia mwezi Februari.

Tathmini ya karibuni ya kila kipindi cha robo mwaka kuhusu madhara kwa raia iliyochapishwa na komandi ya Marekani ya Afrika, (AFRICOM), inathibitisha kwamba vikosi vya Marekani vilifanya mashambulizi ya anga karibu na mji wa Jilib, Februari 15, lakini inakanusha kwamba mashambulizi hayo yaliwauwa madaktari hao.

“Februari 17, 2024, komandi ilipokea ripoti moja ya chanzo cha habari cha mtandaoni ikisema kuwa raia wawili waliuawa kutokana na operesheni ya kijeshi ya Marekani katika eneo la Jilib, Somalia, Februari 15, 2024,” ripoti ya tathmini ya AFRICOM imeeleza.

“Komandi ilikamilisha uchunguzi wa taarifa zilizokuwepo na kuhitimisha kuwa mashambulizi ya anga ya Marekani, ya Februari 15, 2024, halikusababisha madhara kwa raia.”

Forum

XS
SM
MD
LG