Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 16, 2025 Local time: 03:34

Marekani yapanga mashambulizi dhidi ya washirika wa Iran, Mashariki ya Kati


Lloyd Austin, Waziri wa Ulinzi wa Marekani.
Lloyd Austin, Waziri wa Ulinzi wa Marekani.

Vikosi vya Marekani vinapanga kushambulia washirika wa Iran kote Mashariki ya Kati kwa nguvu zaidi, kama majibu wa ya shambulizi la droni kwenye kituo kimoja cha kijeshi nchini Jordan, lililouwa wanajeshi watatu wa Marekani na kujeruhi wengine zaidi ya 40.

Waziri wa Ulinzi wa Marekani Lloyd Austin wakati akizungumza na wanahabari kwa mara ya kwanza tangu alipolazwa hospitalini Januari mosi, kufuatia upasuaji wa kutibu saratani ya tezi dume, ametaja shambulizi hilo kuwa la kutisha, akiongeza kuwa visa kama hivyo havitavumiliwa na Marekani.

“Ni wakati wa kupunguza uwezo wao zaidi ya tulivyofanya awali,” Austin amesema Alhamisi, alipoulizwa ni kwa nini Marekani imechukua muda mrefu kujibu vikali zaidi ya mashambulizi 165 dhidi ya vikosi vya Marekani huko Mashariki ya Kati kufikia kati kati ya Oktoba mwaka jana.

Austin pia alionekana kupuzia taarifa iliyotolewa la Kataib Hezbollah ambalo ni kundi la wanamgambo linaloungwa mkono na Iran, kwamba linasitisha operesheni zake za kijeshi dhidi ya Marekani, akisema, “tunasikiliza kile watu wanasema, lakini tunatazama yale wanayafanya,” na kuongeza kwamba vitendo ndivyo muhimu Zaidi.

Forum

XS
SM
MD
LG