Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Machi 19, 2024 Local time: 11:36

Marekani yamuonya Assad asitumie silaha za kemikali


Rais Bashar Assad
Rais Bashar Assad

Marekani imesema Jumanne huenda kuna matayarisho yanayofanywa na vikosi vya serikali ya Syria ya kutekeleza shambulizi lingine la kemikali dhidi ya raia wake.

Shambulizi la kemikali liliwahi kutekelezwa na serikali ya Syriamnamo mwezi Aprili,Kaskazini mwa nchi hiyo.

Marekani ililazimika kujibu shambulizi hilo la kemikali kwa mashambulizi ya kupitia anagani.

Taarifa iliyotolewa na msemaji wa Ikulu, Sean Spicer, jana Jumatatu ilimuonya rais wa Syria, Bashar Al-Assad, kwamba iwapo serikali yake itatekeleza shambulizi lingine la kemikali, basi yeye na jeshi lake wawe tayari kwa matokeo yatakayokuwa na madhara makubwa.

Hakuna habari zaidi zilizotolewa kuhusu madai hayo ya matayarisho.

Balozi wa marekani kwenye Umoja wa Mataifa, Nikki Haley, aliandika ujumbe kupitia mtandao wa Twitter, kwamba Assad atalaumiwa kwa mashambulizi yoyote mengine dhidi ya raia wa Syria.

Alisema kuwa Russia na Iran, ambazo zimekuwa zikiuunga mkono utawala wa Assad, pia zuitakuwa za kulaumiwa.

XS
SM
MD
LG