Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Januari 25, 2025 Local time: 15:28

Marekani kutumia kura ta turufu kuzuia azimio la Algeria


Kura ya turufu ya Marekani, itaweza kutumika kuzuia mpango wa Algeria, unaotarajiwa kufikishwa mbele ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wiki hii wa kusitishwa mara moja vita vya Israel, vya Gaza, kwa mujibu wa balozi wa Marekani, wa Umoja wa Mataifa.

Linda Thomas-Greenfield, amesema katika taarifa yake Jumamosi kwamba Marekani imekuwa ikifanyakazi kwa miezi kadhaa juu ya suluhisho endelevu la mzozo wa Gaza ambao utaleta kwa haraka na utulivu endelevu kwa Gaza kuanzia angalau wiki sita, na kisha kuchukua hatua za kujenga amani ya kudumu.

Amesema mpango huo ambao Marekani inaufanyia kazi pamoja na Israeli, Misri na mataifa mengine, unawakilisha fursa bora ya kuwaunganisha mateka wote na familia zao na kuwezesha kusitisha mapigano kwa muda mrefu, kuruhusu chakula zaidi cha kuokoa maisha, maji, mafuta, dawa, na vitu vingine muhimu kuwafikia raia wa Palestina wenye uhitaji.

Forum

XS
SM
MD
LG