Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Juni 24, 2025 Local time: 10:53

Marekani kuendelea kuimarisha uhusiano na nchi za Asia


Waziri mkuu wa Singapore Lee Hsien Loong akiwa na rasi wa Marekani Joe Biden katika kikao na waandishi wa habari, Washington Marcg 29, 2022 Picha ya AP
Waziri mkuu wa Singapore Lee Hsien Loong akiwa na rasi wa Marekani Joe Biden katika kikao na waandishi wa habari, Washington Marcg 29, 2022 Picha ya AP

Rais wa Marekani Joe Biden amesema kwamba Marekani inaendelea vizuri na mkakati wake wa kuimarisha uhusiano na mataifa ya Asia-Pacific, licha ya kuwepo mgogoro ambao umesababishwa na uvamizi wa Russia nchini Ukraine.

Akizungumza wakati wa mkutano na waziri mkuu wa Singapore Lee Hsien Loong katika white house, Biden amesema kwamba utulivu wa dunia unakabiliwa na changamoto kadhaa, lakini Washington haijatatizika na vita vya Ukraine.

Biden amesema kwamba anataka kuhakikisha kwamba eneo la Asia pacific ni huru na wazi, hatua ambayo white house inaona kama jaribio la China kutaka kudhibithi eneo hilo kibiashara.

"mipaka haiwezi kubadilishwa kwa lazima, na mataifa yote, makubwa au madogo, yana haki sawa na uhuru, na yana haki ya huo uhuru. Na nataka kukushukuru waziri mkuu na utawala wa Singapore kwa kuunga mkono watu wa Ukraine. Najua kwamba sio rahisi lakini nataka kukushukuru kwa hilo, na umekuwa msitari wa mbele kila wakati umehitajika kufanya hivyo.” Amesema rais Biden

Lee amesisitiza kuhusu ushirikiano mzuri kati ya Marekani na nchi za ASEAN, akisema kwamba utasaidia Marekani kushiriki vikamilifu katika maswala ya Asia-Pacific na kuimarisha zaidi ushirikiano wake na marafiki wengi pamoja na kusimamia maslahi muhimu ya eneo hilo.

XS
SM
MD
LG