Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 16, 2025 Local time: 19:06

Marekani ina wasiwasi wa kushambuliwa na magaidi


FBI Director Christopher Wray testifies before a House Approbations Subcommittee
FBI Director Christopher Wray testifies before a House Approbations Subcommittee

Kuongezeka kwa imani kwa wafuasi wa kundi la kigaidi la Islamic state kulikodhihirika katika mfululizo wa vitisho vya mtandaoni dhidi ya bara la Ulaya pamoja na shambulio baya la kundi hilo kwenye jumba la tamasha nchini Russia, kunawatia wasiwasi maafisa wa usalama wa Marekani.

Maafisa wa usalama wa taifa na vyombo vya sheria wamekuwa na wasiwasi kwa muda mrefu kuhusu makundi madogo au watu binafsi kushawishiwa na njama za ugaidi duniani kote kufanya mashambulizi nchini Marekani.

Lakini mkurengezi wa idara ya upelelezi FBI, Christopher Wray aliwambia wabunge Alhamisi kwamba jambo la kutisha zaidi linaweza kutokea.

“Jambo linalotia wasiwasi zaidi ni uwezekano wa shambulio lililopangwa kufanyika hapa nchini, sawa na shambulio la ISIS-K tuliloona kwenye jumba la tamasha la Russia wiki chache zilizopita,” Wray aliwaonya wabunge.

Siku chache zilizopita, idara za polisi kote barani Ulaya ziliimarisha usalama baada ya vyombo vya habari vyenye uhusiano na Islamic State, kuchapisha jumbe za kushambulia viwanja vinavyoandaa mechi za ligi ya mabingwa barani Ulaya wiki hii huko Madrid, London na Paris.

Forum

XS
SM
MD
LG