Wahusika katika mazungumzo hayo sasa wanaharakisha kumalizia kuuandika mswaada huo.
McCarthy amesema kwamba baraza la wawakilishi litapiga kura Jumatano kufanya uamuzi wa mswaada huo na kutoa fursa kwa baraza la senate kuupitisha kabla ya Juni 5 ili kuhakikisha kwamba Marekani haishindwi kulipa madeni yake.
Hata hivyo mambo mengi yaliyomo kwenye mswaada hayajulikani kwa umma japo pande zote katika bunge zinatarajia kutangaza ushindi wao.
Makubaliano hayo yataiwezesha Marekani kuongeza kiwango chake cha kukopa kwa muda wa miaka miwili ijayo.
Forum