Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Desemba 04, 2023 Local time: 12:52

Mapigano makali kati ya M23 na wanajeshi yanaendelea karibu na Goma


Waandamanaji mjini Goma, DRC wakichoma moto bendera ya Rwanda kwa madai kwamba serikali ya Rwanda inaunga mkono waasi wa M23 wanaopigana na wanajeshi wa serikali. Oct 30, 2022
Waandamanaji mjini Goma, DRC wakichoma moto bendera ya Rwanda kwa madai kwamba serikali ya Rwanda inaunga mkono waasi wa M23 wanaopigana na wanajeshi wa serikali. Oct 30, 2022

Mapigano makali yametokea kati ya wanajeshi wa serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo na waasi wa M23 kaskazini mwa mji wa Goma leo Jumapili. Vyanzo vya habari katika jeshi la DRC vimesema kwamba mapigano makali yanaendelea katika Kijiji cha Mwaro, kilomita 20 kutoka Goma.

Kundi la M23, ambalo wapiganaji wake wanatokea kabila la Watutsi, limekuwa likidhibiti sehemu kadhaa za Kivu kaskazini.

Kundi hilo limetoa taarifa Jumamosi, likilishutumu jeshi la DRC kwa kushambulia ngome zake kwa mabomu, na kuuawa raia 15 wakiwemo Watoto wawili, madai ambayo hajayathibitishwa.

Mapigano hayo yanajiri siku moja baada ya jeshi la Kenya kuingia DRC chini ya makubaliano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, kuisaidia nchi hiyo kupambana na makundi ya waasi.

Uhusiano kati ya DRC na Rwanda umeharibika kufuatia mashambulizi ya kundi la M23, DRC ikisisitiza kwamba waasi hao wanaungwa mkono na Rwanda. Ripoti ya Umoja wa Mataifa ambayo haijawekwa wazi, inasema kwamba Rwanda inawaunga mkono waasi hao.

Rais mstaafu wa Kenya Uhuru Kenyatta anatarajiwa mjini Kinshasa leo Jumapili kuendelea na mchakato wa amani nchini DRC. Ziara yake inajiri siku moja baada ya rais wa Angola Joao Lourenco kukutana na rais Felix Tshisekedi wa DRC, baada ya kutembelea Rwanda ijumaa.

XS
SM
MD
LG