Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 03:10

Mapigano kati ya Jeshi la Congo na waasi wa M23 yaendelea kwa siku ya tatu


Wanajeshi wa DRC wakiwa katika eneo lililofanyika shambulizi Beni, Disemba 26, 2021. (Photo by Sébastien KITSA MUSAYI / AFP).
Wanajeshi wa DRC wakiwa katika eneo lililofanyika shambulizi Beni, Disemba 26, 2021. (Photo by Sébastien KITSA MUSAYI / AFP).

Jeshi la Congo FARDC limendelea na mapigano makali na waasi wa M23 kwa siku yake ya tatu huko Rugari wilayani Rutshuru Kivu kaskazini mashariki mwa Congo,

Waasi walishambulia kambi za jeshi la Congo za Nyesisi kilometa 35 kaskazini mwa Mji wa Goma karibu na mbuga ya wanyamapori ya Virunga.

Eneo hilo lililokuwa na mashambulizi sehemu moja ipo upande wa DRC na sehemu nyingine upande wa Rwanda.

Kanali Ndjike Gylaume msemaji wa jeshi la FARDC Kivu kaskazini ameiambia Sauti ya America kwamba jeshi la Congo linapambana vikali na waasi hao likitumia silaha nzito.

XS
SM
MD
LG