Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Machi 22, 2025 Local time: 08:39

Mandela aaga dunia akiwa na umri wa miaka 95



Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ametangaza Ijumaa usiku kwamba rais wa zamani mpinzani mkuu wa ubaguzi wa rangi Madiba Nelson Mandela amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu. Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ametangaza Ijumaa usiku kwamba rais wa zamani mpinzani mkuu wa ubaguzi wa rangi Madiba Nelson Mandela amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Akilihutubia taifa Rais Zuma alisema "Taifa letu limempoteza mwana wake mkuu shujaa. watu wetu wamempoteza baba yao"

Mandela alikuwa rais wa Kwanza muafrika kuchukua madaraka kutoka kwa utawala wa ubaguzi wa rangi kutoka kwa wazungu walowachache 1994. Kwa wengi alikua shujaa, mtu shupavu na mwenye mtizamo.

Mara kwa mara alikuwa mnyenyekevu, mchangamfu, muaminifu na mtu ambae aliwajali wananchi wote.
please wait

No media source currently available

0:00 0:03:26 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Mwaka 1962, Madiba jina lake maarufu huko Afrika Kusini alikamtwa na kushtakiwa kwa tuhuma za kufanya vitendo vya kutaka kuihujumu serikali. Hata hivyo alijitetea akisema hivyo vilikuwa vitendo vya kuwakomboa waafrika walowengi. Miaka miwili baadae alihukumiwa kifungo cha maisha katika kiswa cha Robben kwenye pwani ya mji wa magharibi wa Cape Town.

Mandela aliachiwa huru miaka 27 badae, ikiwa mwaka 1990 pale serikali ya wazungu wachache iliyokua inaongozwa na Rais Frederik De Klerk kuhalalisha vyama vyote vya kisiasa na kuwafungua wafungwa wote wa kisiasa.

Utawala wa mpito ulienddelea na majadiliano ya kutayarisha katiba na utawala wa kidemokrasia ulianza ukiongozwa na Mandela na De Klerk. Uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vyote na watu wa kabila zote ulifanyika 1994 na Mandela kuchaguliwa akiwa na umri wa miaka 74.

Mandela na mkewe Winnie walikuwa pamoja baada ya kuachiliwa huru kutoka gereza la Robben Island, lakini hai8kuchukua muda wakaachana. Na katika kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwake alipotimiza miaka 80 alimuoa Graca machel, mjane wa rais wa zamani wa Msumbiji Samora Machel.

Alibaki madarakani kwa mhula mmoja wa miaka mitano, na kuanza kampeni chungu nzima moja wapo ikiwa ni kutetea haki za watoto na kupambana na ugonjwa wa Ukimwi. Akiwa madarakani alikosolewa kwa kutokubali kuchukua hatua za nguvu kupambana na janga hilo.

Miaka miwili baada ya kuondoka madarakani mtoto wake wa kiume alifariki kutokana na ukimwi na hapo ndipo aliongeza juhudi zake za kupambana na ugonjwa huo.

Akiwa na umri wa miaka 85 hapo mwaka 1999 Mandela alitangaza kwamba anastahafu kabisa kutoka kazi za umaa lakini aliendelea kufanya kazi kutetea haki za watoto.

Mnamo maisha yake yote alipokea mamia ya tunzo lakini tunzo kuu ni ile ya amani ya Nobel ya 1993aliyopata pamoja na hasimu wake rafiki yake Bw De Klerk.
XS
SM
MD
LG