Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Septemba 29, 2023 Local time: 12:50

Makombora ya Korea Kaskazini ya masafa marefu yalijumuisha ya mwaka 2017-Korea Kusini


Korea Kaskazini Kim Jong Un akifurahi na maafisa wa kijeshi katika kile ambacho vyombo vya habari vya serikali vya nchi hiyo vinakiita kombora la masafa marefu la "Hwasong-17" (ICBM).

Majaribio ya Korea Kaskazini ya makombora ya masafa ya mbali yaliyo fanyika wiki iliyopita, yalijumuisha yale yaliyofanyiwa majaribio mwaka 2017, si aina mpya ya makombora ya kuvuka mabara ambayo Korea Kaskazini imedai kuyafyatua kwa mujibu wa jeshi la Korea Kusini.

Makombora yaliyotumika Machi 24 kuna uwezekano yalikuwa yameboreshwa ya Hwasong-15 ICBM, na si makubwa ya Hwasong-17 ICBM, kwa mujibu wa msemaji wa jeshi la Korea Kusini aliyeongea na Sauti ya Amerika – VOA – siku ya Jumanne.

Televisheni ya taifa ya Korea Kaskazini wiki iliyopita ilitoa video za majaribio zikimuonyesha kiongozi wao Kim Jong Un yeye mwenyewe akielekeza kile kilichodaiwa kuwa majaribio ya hivi karibuni.

XS
SM
MD
LG